Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Polisi wakomaa na dereva wa Lissu

Jumatatu , 11th Sep , 2017

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Nchini DCI Robert Boaz amemtaka dereva wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kufika polisi kwa ajili ya mahojiano juu ya tukio la kupigwa risasi kwa kiongozi huyo ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Nchini DCI Robert Boaz

Mkurugenzi huyo amesema hayo leo wakati akifanya mahojiano na kipindi cha HOTMIX  ambapo amesema "Polisi inaendelea kumtaka dereva huyo kufika kwa ajili ya kuisaidia Polisi katika uchunguzi wa tukio hilo".

Hata hivyo kuhusiana na dereva huyo (Simon Bakari), Mwenyekiti wa (CHADEMA) Freeman Mbowe jana katika taarifa yake alisema kutokana na dereva huyo kushuhudia tukio la kutisha wameamua kumpeleka Nairobi ili kupatiwa huduma za kisaikolojia 

Akizungumzia muitikio wa viongozi na watendaji mbalimbali wanaoendelea kufika katika Jeshi hilo kwa ajili ya mahojiano baada ya kutajwa katika taarifa mbili za Kamati za Bunge zilizochunguza Sekta ya Madini ya Almasi na Tanzanite, DCI amekiri kuridhishwa.

DCI Boaz amesema viongozi hao wamekuwa wakifika kwenye  kikosi maalum cha upelelezi ambacho kimeundwa na vikosi vyote vya Upelelezi, na kuongeza kuwa wanaendelea kuhojiwa na kwa wale watakaobainika kuhusika watapelekwa Mahakamani.

Amesema viongozi hao pamoja na wengine watakaofika wataendelea kuhojiwa kufuatia amri ya Amiri Jeshi Mkuu na kufuatiwa na wito wa Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro aliyetaka viongozi hao kufika kwa ajili ya mahojiano baada ya kutajwa kwenye taarifa za kamati hizo mbili.

 

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera