
Msanii wa Muziki wa nchini Uganda Phina Mugerwa akiwa na mtoto wake
Phina tayari amekwishaanza kushiriki furaha yake hii na mashabiki wake mitandaoni kwa kuweka picha za Ken akiwa na mtoto wao kuonesha kuwa baba amerudi nyumbani, na vilevile kuthibitisha usemi wake kuwa hakuna mwanamke anayeweza kumuibia mwanaume wake.
Mpaka sasa hakuna tamko rasmi kutoka kwa Cindy wala Ken kuhusiana na kutengana kwao, ikikumbukwa kuwa wawili hawa walikwishafikia mpaka hatua ya kwenda kutambulishana kwa wazazi, wakiwa na matarajio makubwa ya kufunga ndoa baadaye.
