Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nay amjibu Mwakyembe

Jumatatu , 22nd Mei , 2017

Rapa Nay wa Mitego amefunguka na kumtaka Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe kutoa ufafanuzi juu ya kauli yake aliyotoa kuwa wasanii wasijihusishe na masuala ya siasa. 

Nay wa Mitego akiongea kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio, amesema kuwa yeye anaamini muziki ni siasa na siasa ni muziki hivyo ni ngumu kutofautisha vitu hivyo viwili, hivyo amemuomba Waziri mwenye dhamana kutoa ufafanuzi juu ya kauli hiyo na kudai yeye hajawahi kuimba wimbo wa siasa bali anaimba mambo yaliyopo kwenye jamii. 

"Nachoamini mimi muziki ni siasa na siasa ni kama muziki, siasa ni maisha ya watu ambayo wanaishi kila siku na muziki pia ni maisha ya watu ambayo wanaishi kila siku kwa hiyo anahitaji kutoa ufafanuzi wa kutosha juu ya hili. Siasa ni maisha ya watu na muziki ni maisha ya watu, mimi binafsi naamini sijawahi kuimba wimbo wa siasa hata siku moja bali ninaimba maisha ya watu ambayo yanaendelea kila siku na ndiyo maana wengi wanathubutu kusimama upande wangu endapo linatokea tatizo lolote" alisema Nay wa Mitego.

Mbali na hilo Nay aliendelea kusisitiza kuwa kuna haja Waziri kutoa ufafanuzi wa jambo hilo 

"Mh. Waziri anatakiwa kutoa ufafanuzi juu ya jambo hili ili watu wajue kipi hawatakiwi kuimba na kipi wanatakiwa kuimba sababu siasa ni maisha ya watu ya kila siku na muziki wa Hip hop ni maisha ya watu ya kila siku, kwangu mimi muziki wangu hauwezi kubadilika zaidi nitazidi kuongeza vitu ili nisiwaudhi watu na nizidi kuongeza idadi ya mashabiki" alisisitiza Nay wa Mitego

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria