Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

FAINALI DANCE 100% 2015 KUWASHA MOTO JUMAMOSI

Jumatatu , 12th Oct , 2015

Mashindano makali ya kucheza yaliyojizolea umaarufu mkubwa Afrika Mashariki Dance 100% 2015 yanafikia tamati jumamosi hii, ambapo mshindi wa fainali hizi mwaka huu atabeba kitita cha shilingi milioni 5 za Tanzania pamoja na zawadi nyingine.

Akipiga stori na mwandishi wa habari, mtayarishaji wa kipindi cha Dance 100% kinachorushwa na EATV kila jumamosi saa kumi na mbili na nusu jioni Ndimbuni Msongole, amesema fainali za mwaka huu zitakua na mvuto kwani ni makundi matano tu yamebaki kati ya makundi hamsini.

“Mwaka huu kutakua na good show (onyesho zuri) watu wategemee vitu vizuri kwani hakuna utabiri nani atakua mshindi makundi yalikua hamsini, lakini sasa yamebaki matatu kwa hiyo washiriki watatumia uwezo wao binafsi,” alisema Ndimbuni.

Naye mtangazaji machachari wa mashindano haya ya Dance 100% yanayoandaliwa na East Africa Television na East Africa Radio, TBway 360 amezungumzia tofauti ya fainali za mwaka huu na miaka iliyopita.

“Kuna tofauti kati ya mashindano ya miaka ya nyuma na mwaka huu kwa sababu makundi mengi yamerudi baada ya kushiriki mashindano ya miaka iliyopita hivyo washiriki wengi wana uzoefu mkubwa hali inayoleta fainali yenye ushindani zaidi,” alifunguka mtangazaji huyo.

Makundi yaliyofanikiwa kuingia fainali ni fainali za Dance 100% 2015 ni The WD, Team Makorokocho, Best Boys Kaka Zao, The Winners Crew pamoja na Team ya Shamba. Fainali hizo zitatimua vumbi jumamosi hii ya tarehe 10 saa nane mchana katika viwanja vya Don Bosco Oysterbay Jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera