Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Alikiba aahidi kufanya kazi na 'madansa' #Dance100

Jumapili , 25th Sep , 2016

Msanii wa Bongo Fleva Alikiba ameahidi kuchukua baadhi ya vijana walioshiriki hatua ya fainali ya shindano la Dance100% 2016.

Msanii Ali Kiba ambaye ameshiriki kama jaji mgeni Dance100%

Akizungumza na EATV Alikiba amesema uwezo uliooneshwa na makundi yaliyoshiriki umemfanya aone kuna sababu ya msingi ya kukuza vipaji vyao kwa kuchukua baadhi ya waliofanya vizuri na kuwajumuisha kwenye kazi zake.

“Nashukuru kwa kuwa Jaji mgeni katika hatua hii ya fainali, jambo ambalo limenifanya nione namna ambavyo kuna vipaji vingi sana katika jamii yetu na kuna baadhi ya vijana nitawachukua kufanya nao kazi katika shughuli zangu za muziki” Amesema Alikiba

Aidha ameupongeza uongozi wa EATV kwa namna ambavyo umebuni namna ya kukuza vipaji vya wasanii kwa kuanzisha shindano la Dance100% maana kuna vipaji vingi sana ambavyo vinavumbuliwa na wengi wanaweza kupata ajira na kutambulika kupitia Dance100%.

Pamoja na hayo Alikiba amewataka washiriki ambao wameshindwa kushika namba moja au mbili wasikate tamaa kwani katika maisha kujituma ni njia ya kupata mafanikio.

Shindano la Dance100% 2016 limefikia hitimisho leo kwa makundi 6 kupambana ambapo kundi la Team Makorokocho limeibuka na ushindi na kujinyakulia kitita cha milioni 7.

Matukio yote ya Dance100% yataoneshwa kupitia kituo cha EATV siku ya Jumapili kuanzia saa moja jioni ambapo shindano limedhaminiwa na Vodacom kwa kushirikiana na Coca- Cola.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine