Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ziara ya kushtukiza RC Dar, maagizo makali Ilala

Jumapili , 18th Oct , 2020

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge, amefanya ziara ya kushtukiza usiku wa kuamkia leo Oktoba 18, 2020, kwenye Ujenzi wa Machinjio ya kisasa Vingunguti, Soko la Kisutu na Stendi ya kisasa Mbezi Louis na kubaini kwenye Machinjio ya Vingunguti na Soko la Kisutu, wakandarasi

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge

hawafanyi kazi usiku na mchana kama alivyowataka.

Kunenge amesema kukiukwa kwa agizo la kufanya kazi usiku na Mchana kumepelekea miradi hiyo kushindwa kukamilika ndani muda uliopangwa na kuleta kero kwa wananchi.

Kutokana ukiukwaji wa maagizo yayo RC Kunenge ametoa maagizo matatu mazito kwa Manispaa ya Ilala ikiwemo kuhakikisha Mkandarasi anapigwa faini kwa kushindwa kukamilisha ujenzi ndani ya muda kwa mujibu wa mkataba, Kumchukulia hatua za kinidhamu Msimamizi wa Mradi pamoja na kumuwajibisha Mhandisi Manispaa hiyo kwa kushindwa kusimamia kazi yake.

Aidha RC Kunenge amemuelekeza Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kumpatia mapendekezo ya jinsi gani watakamilisha miradi hiyo kwa haraka ili iweze kuwa msaada kwa wananchi.

Ukiacha Soko la Kisutu na Machinjio ya Vingunguti, kwenye ujenzi wa Stand Mpya ya Mbezi Louis RC Kunenge amekuta kazi inafanyika usiku na Mchana, ikiwa ni utekelezaji wa Agizo la Rais Dkt. John Magufuli alilotoa wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi na kuagiza Mradi ukamilike kabla ya mwishoni mwa mwezi Novemba.

RC Kunenge amesema leo Oktoba 18 jumla ya Makontena 13 yenye Vifaa vya Ujenzi wa Stand ya Mbezi yaliyokuwa yamekwama bandarini yataanza kutoka baada ya kufanya mazungumzo na viongozi wa Wizara na Mamlaka ya Mapato TRA.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya