Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanafunzi kupimwa 'TB' kwa lazima

Ijumaa , 24th Mar , 2017

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amepiga marufuku shule za binafsi na serikali kupokea wanafunzi bila kupimwa ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB)

Ummy Mwalimu

Pia Waziri Ummy ameagiza watu walio katika makundi hatarishi wakiwemo wanaoishi na maambukizi ya UKIMWI na wajawazito wafike vituo vya Afya kupimwa Kifua Kikuu (TB).

"Ni marufuku kwa Shule za bweni za umma na binafsi pamoja na vyuo kupokea mwanafunzi ambaye hana uthibitisho wa kuchunguzwa ugonjwa wa TB. Hatutamvumilia Daktari/Mganga atakae-sign na kutoa Cheti cha Uchunguzi wa Magonjwa ukiwemo Ugonjwa wa TB kwa Mtu ambae hajafanyiwa Uchunguzi". Amesema Ummy

Akitoa maagizo hayo leo Jijini Arusha kwenye maadhimisho ya siku ya Kifua Kikuu Duniani, Ummy alisema lengo la kupima makundi hayo muhimu ni kuzika kuenea kwa ugonjwa huo mapema, kwani mgonjwa mmoja ana uwezo wa kuambukiza watu 20 kwa mwaka kama hajaanza kutumia dawa kitu ambacho ni hatari.

Bweni ya wanafunzi

"Makundi hatarishi ambayo lazima wapimwe wale wanaoishi na Virusi vya Ukimwi, watoto chini ya miaka mkutano, wajawazito, wafungwa, watumiaji madawa ya kulevya, watu wanaougua saratani na kisukari lazima wapime Kifua Kikuu kwa lazima," amesema

Alisema tatizo ni kubwa nchini kwani takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa Tanzania kwa mwaka 2015 jumla ya watu 160,000 waliugua Kifua Kikuu kati ya hao watu 62,180 sawa na asilimia 39 tu ndiyo waligunduliwa na kupata matibabu.

"Hii inamaanisha katika kila watu 100,000, watu 306 wanaougua ugonjwa wa Kifua Kikuu kila mwaka nchini na kati ya hao wanaougua inakadiriwa watu 55,000 duniani wanafariki dunia kila mwaka," amesema

Amesema Mkoa wa Dar esalaam bado unaongoza kuwa na idadi kubwa yawagonjwa wa kifua kikuu ambapo waliopo ni asilimia 22, ikifuatiwa na Mwanza, Mbeya, Morogoro, Shinyanga, Arusha, Mara, Manyara, Tanga na Kilimanjaro.

"Mikoa hii pamoja na Daresalaam huchangia asilimia 63 ya wagonjwa wote waliogundulika nchini mwaka 2015," amesema

Amesema kutokana na hilo serikali imeweka mkakati kuongeza vituo vyenye mashine za kisasa za kupima kifua kikuu kutoka mashine 70 hadi kufika mashine 150 ifikapo Desemba  2017 ambapo mashine hizo kila moja ina uwezo wa kupima wagonjwa 12 kwa siku na ifikapo Juni 2018 hospitali za Wilaya na Mikoa zitakuwa na mashine hizo zenye uwezo wa kutoa majibu ndani ya saa mbili.

 

 

HABARI ZAIDI

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera