Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wahamiaji haramu 2,935 wakamatwa Kagera

Alhamisi , 4th Aug , 2022

Jumla ya wahamiaji haramu 2,935 wamekamatwa na idara ya uhamiaji katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Kagera, katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Juni mwaka huu, baada ya kubainika kuingia nchini bila vibali

Kamishna Msaidizi Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kagera, Thomas Fussy

Akizungumza na waandishi wa habari Kamishna msaidizi idara ya Uhamiaji Mkoani Kagera, Thomas Fussy amesema kuwa wahamiaji hao haramu wamekamatwa kufuatia oparesheni mbalimbali zinazoendelea kwa lengo la kuwabaini watu hao, na kuwachukulia hatua za kisheria.

"Wahamiaji haramu waliokamatwa kutoka Burundi ni 2,389, Uganda 308, Rwanda 175, Kongo 40, Kenya 10, Ethiopia watano, Somalia watatu, China watatu na Zambia na Zimbabwe mhamiaji mmoja kwa kila nchi, kati ya watuhumiwa hao wahamiaji 2,730 waliondoshwa nchini, 183 wamefikishwa mahakamani na 22 wamehalalisha ukazi wao hapa nchini na kulipa ada kwa hati maalumu" amesema Fussy.

Aidha kutokana na mkoa wa Kagera kupakana na nchi nyingi na kusababisha kuwepo kwa mwingiliano wa watu kutoka katika mataifa hayo, kamishna huyo msaidizi wa idara ya uhamiaji mkoani Kagera amewataka watendaji wa vitongoji, vijiji na mitaa, kutotoa barua za utambulisho kwa wananchi ambao hawana uhakika kama ni wakazi wa maeneo yao, ili kuepuka kutoa nyaraka za serikali kwa watu wasio raia.

"Kwa hiyo mtendaji asikubali kutoa nyaraka kwa mtu ambaye hajamfahamu kwa sababu nyaraka zinaishi, na akiulizwa popote ataonyesha hizo nyaraka na ikibainika sio raia atachukuliwa hatua yeye, na wewe uliyesaini utawajibishwa" amesema Fussy

Nao baadhi ya wananchi waliozungumzia suala hilo wameiomba serikali kupitia mamlaka zake ikiwamo idara ya usalama wa taifa na uhamiaji, kuongeza umakini kuwadhibiti watu wasio raia kuingia nchini bila utaratibu, wakidai wao kama wananchi sio rahisi kuwabaini.

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera