Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Waha wanachapa kazi nchi nzima"- Profesa Lipumba

Jumanne , 22nd Sep , 2020

Mgombea urais kupitia Chama cha Mwananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba, amesema kuwa endapo atapata ridhaa ya kuongoza nchi atahakikisha anatatua tatizo la maji na miundombinu ya barabara za vijijini ili kuhakikisha wakulima wanasafirisha mazao yao kwa urahisi.

Profesa Ibrahim Lipumba

Kauli hiyo ameitoa hii leo Septemba 22, 2020, kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya jumba la maendeleo wilaya ya Kibondo, na kuongeza kuwa ubovu wa miundombinu ndiyo chanzo cha wananchi kuwa na hali ngumu.

"Tujenge miundombinu, barabara za kwenda vijijini zinapunguza gharama za usafirishaji wa mazao kutoka vijijini, Oktoba 28 mkinichagua mimi kipaumbele changu katika ujenzi wa miundombinu itakuwa barabara hii ya Nyakanazi mpaka Kasulu, na maji ya uhakika yaweze kupatikana Kibondo", amesema Profesa Lipumba.

Aidha Profesa Lipumba ameongeza kuwa,"Watani zangu waha wanajulikana nchi nzima ni wachapakazi wa kweli na wakijengewa mazingira mazuri wataboresha kilimo chao, bila kilimo kilicho bora huwezi ukawa na mapinduzi ya viwanda".

Awali akizungumzia suala la maji Profesa Lipumba amesema , wananchi wa Kibondo wamekuwa wakikabiliwa na tatizo la maji pamoja na kubambikiwa madeni na kuahidi kuwa endapo chama chake kitapata ridhaa kitahakikisha wanakuwa na maji yakutosha.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine