Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

SUA wampa tuzo Jafo kwa kuleta tija kwenye jamii

Ijumaa , 25th Nov , 2022

Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kimetoa tuzo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo kwa kutambua na kuthamini mchango wake mkubwa wakati akiwa mwanafunzi chuoni hapo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo, akipokea tuzo

Dkt. Jafo ni miongoni mwa wanazuoni wachache waliopata tuzo hiyo akifanya vizuri katika masomo yake na kuleta tija na mchango mkubwa kwa jamii tangu ahitimu masomo yake chuoni hapo mwaka 2001.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka chuoni hapo, ameipata tuzo hiyo kutokana na mchango wake mkubwa kwa jamii alioufanikisha wakati alipokuwa anatimiza majukumu yake katika jamii kwa vipindi tofauti kutokana na chuo hicho kufuatilia mwendendo na tabia za wanazuoni wao waliohitimu chuoni hapo ili kubaini mchango wao katika jamii. 

"Hii ni heshima kubwa sana kwangu, familia yangu na Taifa langu, niliwahi kusoma hapa miaka iliyopita katika ngazi ya shahada na wanafunzi wapo wengi sana lakini waliona wanipatie mimi hasa kwa mchango mkubwa nilioutoa katika nyanja mbalimbali wa jamii," amesema Dkt. Jafo.

Aidha, Dkt. Jafo ametajwa kuwa ameleta mchango mkubwa alipokuwa katika nafasi ya mtaalamu wa kilimo wa Halmashauri ya Kisarawe mkoani Pwani kwa mwaka 2001 hadi 2005.

Pia taarifa ya chuo hicho imeonesha kwamba alikuwa Mtanzania wa kuigwa kwa kuchapa kazi kwa kuleta matokea alipokuwa akifanya kazi katika Shirika la Kimataifa la Plan International Ofisi ya Tanzania kwa nafasi ya Meneja wa Miradi.

Katika nafasi ya ubunge amehudumia vyema wananchi wake sambamba na kuliwakilisha Bunge la Tanzania katika Bunge la Jumuia ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ikiwa ni pamoja na kuwa Mweka Hazina wake.

Eneo lingine kubwa lililompa heshima hiyo ni kuwa kiongozi mwenye ari, mnyenyekevu, na anaye jituma kwa moyo mkubwa bila ya kuchoka kwa ajili ya jamii alipokuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) na katika nafasi yake ya sasa ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria