Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkutano mkubwa wa uwekezaji kufanyika Dar kesho

Jumanne , 4th Nov , 2014

Tanzania kesho itakuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa kuhusu uwekezaji, ambapo takribani wawekezaji Hamsini wenye mtaji mkubwa wa pesa watakutana na Watanzania ambao ni wamiliki wa makampuni yanayotafuta pesa kwa ajili ya uwekezaji.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini Tanzania Dkt Godfrey Simbeye.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini Tanzania – TPSF, Dkt Godfrey Simbeye, amesema hayo jijini Dar es Salaam leo, na kufafanua kuwa mkutano huo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya TPSF ya kuanzisha mfumo wa mitaji ya ubia kwa ajili ya kukuza fursa za uwekezaji.

Kwa mujibu wa Dkt Simbeye, wawekezaji hao wana mtaji wa fedha zinazozidi shilingi za Kitanzania Trilioni Themanini, ambazo watakuwa tayari kuzitoa kwa miradi iliyobuniwa na wafanyabiashara wa Kitanzania, kupitia utaratibu wa miradi ya ubia baina ya wawekezaji hao na wale wa ndani.

Dkt Simbeye amesema hii ndiyo fursa pekee kwa wafanyabiashara wa Tanzania waliokuwa wanatafuta mikopo ya kufadhili biashara zao, kuchangamkia fursa ya kukutana na wafanyabiashara wanaoutafuta mahali pa kukopesha fedha zao.

Mkurugenzi huyo wa TPSF ameongeza kuwa hii ndiyo nafasi ya watanzania wenye ndoto ya kuanzisha miradi mikubwa ikiwemo viwanda vya magari na ambao walikuwa hawajui wapi watapata kiasi kikubwa cha pesa za kugharamia miradi yao.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali