Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Magufuli amkumbuka Makonda kwa hili

Jumanne , 13th Oct , 2020

Mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli, amesema kuwa mtu wa kwanza aliyeomba ujenzi wa Hospitali ya wilaya ya Ubungo ni aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, na ndipo ujenzi huo ulipoanza.

Kushoto ni aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kulia ni mgombea urais kupitia CCM Dkt John Magufuli.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Oktoba 13, 2020, wakati akiomba kura kwa wakazi wa Ubungo na Kibamba, ambapo amewataka wasifanye makosa ya kumchanganyia na badala yake wachague madiwani na wabunge kutoka CCM.

"Hospitali ya wilaya ya Ubungo mnakumbuka siku ile tupo kwenye sherehe Airport, iliombwa na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, mpaka RC anaomba mbunge alikuwa wapi kuomba, tukaijenga kwa sababu Ubungo na Kibamba ilikuwa kama watoto yatima, msiendelee kuwa yatima", amesema Dkt Magufuli.

Katika hatua nyingine Dkt Magufuli amesema kuwa endapo Ubungo na Kibamba watamchagulia madiwani na wabunge kutoka CCM, atahakikisha anajenga makao makuu ya wilaya ya Ubungo kama ilivyo Kigamboni.

"Tupeni kura, msinikatishe tamaa ndugu zangu aombaye hupewa tumebembeleza mno basi mtupe, na anayepewa lazima ameoma ndiyo maana tumekuja hapa kwa unyenyekevu, mniletee madiwani wa CCM mniletee vijana hawa wawili Profesa Mkumbo na Mtemvu, mkiniletea hawa hamtajuta", ameongeza.

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya