Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Maabara ya Taifa yaondolewa jukumu la COVID-19

Jumamosi , 27th Feb , 2021

Maabara ya Taifa imeondolewa katika orodha ya chaguo (option) la vituo vya kutolea sampuli za kupima COVID -19 kwa njia ya RT - PCR kwa wasafiri katika mfumo wa kutuma miadi wa pimacovid.moh.go.tz. 

Mfano wa sampuli iliyochukuliwa kwaajili ya kufanyiwa vipimo vya Covid-19.

Kwa mabadiliko hayo, kuanzia Machi Mosi, 2021, wasafiri wote wanaohitaji kipimo hiki wanaelekezwa kupata huduma ya kuchukulia sampuli katika Vituo / hospitali za Mjini Dar es Salaam na Mikoani kote (ona kiambatanisho) na baadae kutumiwa vyeti kwa njia ya mfumo wa TEHAMA. 

Maelekezo hayo yametolewa leo na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, tangazo lililosainiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini (Afya), Gerard Chami ambaye  amesisitiza haitaruhusiwa tena wasafiri kwenda moja kwa moja Maabara Kuu iliyoko Mabibo Dar es Salaam, kwa ajili ya kipimo au majibu au vyeti.

 "Lengo ni kuongeza ufanisi wa majibu na kuondoa mrundikano wa wasafiri katika maabara kuu," amebainisha, Maabara ya Taifa imekuwa ikichukua sampuli, ikizichakata, kuzipima, kutoa majibu pamoja na kuandaa vyeti kwa wasafiri  katika kutekeleza jukumu hilo, kumekua na wasafiri wengi wanaofika kwenye Maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii na kusababisha msongamano mkubwa katika eneo la maabara”, imesema taarifa ya Wizara

 Kwa mabadiliko mapya, Chami amesema wasafiri wanakumbushwa tena kuchukuliwa sampuli siku tatu (masaa 72) kabla ya kusafiri ili kuepuka kuchelewa kwa vyeti. 

"Wasafiri wote watatakiwa kwenda kwenye vituo vya kuchukulia sampuli kama ilivyotolewa kwenye Mwongozo wa Ushauri kwa Wasafiri (Travellers Advisory). Hivyo kuanzia tarehe 01 Machi, 2021 Maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii haitapokea wasafiri na kuwachukua sampuli na badala yake itabaki na jukumu la kupiman kutoa vyeti ikiwa ndio jukumu lake la msingi," amesisitiza Chami.

HABARI ZAIDI

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera