Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kijana ahukumiwa miaka 30 kwa kubaka mtoto

Jumatano , 25th Mei , 2022

Mahakama ya wilaya ya Iringa, imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela Jofrey Mtokama (21), mkazi wa Kijiji cha Igluba mkoani Iringa baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mtoto wa miaka 9, huku Jamhuri ikipinga adhabu iliyotolewa ni ndogo ukilinganisha na ukubwa wa kosa.

Jofrey Mtokama, aliyehukumiwa miaka 30 jela

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mwandamizi Emmy Nsangalufu, amesema Mtokama mkazi wa wa Kijiji cha Igluba wilayani Iringa amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na kulipa faini ya shilingi laki tano kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka 09.

Akisoma maelezo mbele ya Hakimu huyo, mwendesha mashtaka Alice Thomas, akisaidiana na Jackline Nungu, amesema kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa mnamo tarehe Mei 13, 2021 katika kijiji cha Igluba wilayani Iringa, mkoa wa Iringa.

Amesema kuwa mhumiwa huyo ambaye  kazi yake ni  kuchunga Ng’ombe alienda nyumbani kwa mtoto huyo usiku baada ya kugundua kwamba wazazi wa mtoto huyo walikuwa kwenye sherehe ya pombe kijijini hapo na kumrubuni kwamba anaitwa na mama yake.

Thomas aliielezea Mahakama kwamba baada ya kufanikiwa kumdanganya mtoto alimpeleka sehemu na kumbaka na kumsababishia maumivu sehemu zake za siri na kutokomea porini baada ya wazazi wa mtoto kurudi toka kwenye sherehe, mtoto huyo alimwambia mama kilichotokea na alipomchunguza sehemu zake za siri hizo alikuta damu zinatoka.

Baada ya hapo zoezi la kumsaka kijana huyo lilipoanza usiku wa manane na kufanikiwa kumkata akiwa amejificha kichakana karibu na pori la kijiji na kumpeleka katika serikali ya kijiji na hatimaye kumpeleka polisi na kesi ikafunguliwa.
 

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria