Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

JPM awaongoza watanzania siku ya Mashujaa

Jumanne , 25th Jul , 2017

Rais John Magufguli, leo Julai 25, amewaongoza watanzania kwa ujumla, ikiwa pamoja na wananchi wa Singida  waliohudhuria uzinduzi wa barabara ya Manyoni, kuwakumbuka mashujaa wa taifa hili waliopambana katika vita mbalimbali ikiwemo vita ya Kagera.

Dkt. Magufuli aliwataka watu waliohudhuria mkutano huo wa hadhara kusimama kwa dakika moja ili kutoa heshima kwa mashujaa hao kwakuwa leo ni siku ya mashujaa ambayo huadhimishwa kila ifikapo Julai 25.

Kupitia hadhara hiyo Magufuli amevipongeza vikosi vyote vya majeshi ya ulinzi na usalama nchini kwa kazi kubwa wanayofanya, kuilinda nchi na kuifanya kuwa tulivu kiasi cha kuwavutia watu wengine kukimbilia kujiunga na vikosi vya jeshi.

Katika hatua nyingine Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) limeadhimisha Siku ya Mashujaa kwa kutoa huduma za afya, kuchangia damu na kufanya usafi wa mazingira katika maeneo mbalimbali nchini katika kuwakumbuka na kuwaenzi waliopoteza maisha wakishiriki vita mbalimbali kutetea nchi yao.

Akizungumza na vyombo vya Habari katika viwanja vya Mnazi Mmoja leo Jijini Dar es Salaam, ambako maadhimisho hayo yamefanyika kimkoa, Mkuu wa Majeshi nchini Jenerali Venance Mabeyo amesema, "huduma za jamii zilizotolewa hii leo zinalenga kusogeza jeshi hilo karibu zaidi na wananchi wake sambamba na kuhakikisha mahitaji muhimu ya kiafya hususani upatikanaji wa damu salama ni uhakika".
 

HABARI ZAIDI

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera