Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Filamu ya Royal Tour yaoneshwa Korea Kusini

Jumamosi , 25th Jun , 2022

Bodi ya Utalii Tanzania kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Korea Kusini imetumia maonesho ya Seoul International Tourism Expo (KOTFA 2022), kuonesha Makala ya The Royal Tour Tanzania kwa Mawakala wa utalii pamoja na Waandishi wa habari za utalii katika soko ya utalii nchi hiyo.

Maonesho yameanza tarehe 23 – 26, 2022.

“Nashukuru leo tumefanikiwa kukutana na wadau wa utalii wa hapa Korea Kusini, huu ni mwanzo mzuri na tutaendelea na utaratibu huu ili wadau waweze kuvijua zaidi vivutio vya utalii vya Tanzania. Baada ya kuona filamu ya The Royal Tour, TANZANIA, wamependa kujua fursa za uwekezaji zilizopo Tanzani, jambo ambalo linaleta matumaini kwa Mawakala wa utalii wa nchi hii kuanza kuuza utalii wa Tanzania.

Hayo yamesemwa na  Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Balozi Togolani Edriss Mavura wakati wa mkutano  uliofanyika Juni 24, 2022 katika hotel ya Intercontinental Seoul Pama iliyopo  katika mji wa Seoul.

Naye Afisa Habari na Uhusiano wa Bodi ya Utalii Tanzania, Bi.  Augustina Makoye ametumia mkutano huo kuwakaribisha wawekezaji kutoka Korea Kusini kwani Tanzania bado ina fursa za uwekezaji katika sekta ya utalii hasa kwa upande wa  Malazi, Migahawa na huduma nyingine, ili iwe chachu ya kuwavutia watalii wengi kutoka katika soko la utalii la Korea.

Aidha, wakati anatoa neno la shukrani, Bi. Augustina ametumia muda huo kuwaalika Mawakala wa utalii wa Korea Kusini kushiriki Onesho la Utalii la Swahili International Tourism Expo (SITE) linaloandaliwa na Bodi ya Utalii Tanzania. Onesho hilo limepangwa kufanyika wiki ya mwisho ya mwezi Oktoba 2022 jijini Dar es Salaam, na ameahidi kuwatumia mwaliko punde maandalizi ya onesho hilo yatakapo zinduliwa rasmi. 

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria