Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Daktari asimulia A-Z kuhusu muuguzi aliyeuawa

Ijumaa , 25th Mei , 2018

Mwanamke mmoja anayejulikana kwa jina la Rose Mary Magombola ambaye alikuwa muuguzi Mkuu msaidizi wa hospitali ya Mkuranga ameuawa na mtu aliyetajwa kuwa ni mume wake, na kisha mwili wake kufukiwa pembezoni mwa nyumba yao.

Akizungumza na wwww.eatv.tv Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya Steven Mwandambo, amesimulia jinsi tukio hilo lilivyokuwa mara baada ya kuingiwa na hofu kwa kutomuona kazini bila taarifa, na mpaka pale ilipobainika kuwa mume wake alimuua na kumfukia.

“Siku ya tar 21 Jumatatu hatukumuona dada Mary Magombolwa akiwa kazini sasa tulitaka kujua kwa nini kwa sababu sio kawaida yake kutokuja kazini bila taarifa, baadaye tukaona kwa sababu labda ya uchovu labda alichoka tukahisi labda baadaye anaweza akaja, tukalisahau siku ikapita, Jumann asubuhi tulipomkosa tena ikabidi tuanze utaratibu wa kutafuta nini kinaendelea, tuende nyumbani kwake kumuuliza mumewe kama amemuona au ana shida yoyote zaidi mpaka haonekani, lakini kabla hatutatoka hospitali, mume wake alifika na kutuuliza kama mke wake amefika kazini, sasa tulipata utata kidogo maana tulitegemea yeye ndio atupe majibu”, amesema Dk. Mwandambo.

Dk. Mwandambo ameendelea kwa kusema kwamba …... “sisi tukasema huku hajafika tangia jana na tulikuwa tunakuja kwako kukuuliza, kwa sababu na wewe hujui ni bora ukaenda polisi uende ukatoe tarifa, tukamsindikiza akatoa taarifa, na upelelezi ukaanizia pale kwa ajili yakumtafuta, na polisi wakafanya kazi, yeye mwenyewe akawekwa ndani kwa ajili ya kusaidia uchunguzi, na jana ndio ikajulikana kuwa alikuwa ameuawa na kufukiwa katika eneo la nyumba yake”.

Taarifa zaidi zinasema kwamba baada ya upelelezi wa kina mume wa nesi huyo ambaye jina lake halikuwekwa wazi kwa haraka, aliweka wazi kuwa amemuua mke wake na kumfukia karibu na eneo la nyumba yao.

Jeshi la Polisi lilifika eneo la tukio kufukua mwili wa nesi huyo, na kisha kwenda kufanyiwa uchunguzi na kutangazwa kuwa utazikwa mapema hii leo.

 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine