Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera, Maketi Msangi
Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera Maketi Msangi, na kusema kwamba tukio la mauaji hayo lilitokea Mei 20, 2022.
"Walimjeruhi vibaya Pankras kwa kumkata na kitu cheye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake, alikimbizwa hospitali ya Mission ya Isingiro na alifariki siku hiyo akipatiwa matibabu, watuhumiwa hao walikimbilia kusikojulikana, tulianza msako na kuwakamata Mei 25 baada ya kupata taarifa za siri," amesema Msangi.