Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

53 wafariki kwa kipindupindu Dar es salaam

Jumamosi , 7th Nov , 2015

Takribani watu 53 wamekufa katika jiji la Dar es salaam tangu kuanza kwa ugonjwa wa kipindupindu miezi mitatu iliyopita.

Mratibu wa magonjwa ya milipuko kutoka wizara y Afya na ustawi wa jamii Bi. Victoria Bura amesema hayo leo jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kutoa tathmini ya ugonjwa huo.

Amesema kwa sasa wilaya ya Temeke ndio inaongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi wa kipinudupindu ambapo kuna wagonjwa 39, Ilala mgonjwa 1 na Kinondoni mgonjwa 1.

Wakati hali ikielezwa kuwa mbaya, mama lishe katika soko la samaki la Feri jijini humo wamelalamikia kukosekana kwa maji safi katika soko hilo na hivyo kulazimika kupikia kwa kutumia maji ya chumvi kufuatia kukatwa kwa maji kunakotokana na deni linalodaiwa na kampuni ya maji safi na maji taka DAWASCO.

Kufuatia hali hiyo mama lishe hao wamesema sasa wamekuwa wakilazimika kununua maji kwa shilingi elfu moja hadi elfu mbili kwa dumu moja la lita ishirini huku wakieleza kukosekana kwa uhakika wa usalama wa vyakula vinavyopikwa kwa kutumia maji ya chumvi.

Wakati huohuo baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es salaam wameelezea kusikitishwa kwao na tatizo la mara kwa mara la utiririshaji wa maji taka unaotokana na chemba ya maji taka katika barabara ya Upanga.

Wakieongea na KURASA leo wakazi hao wamesema tatizo hilo linatokana na kutokuwa na mipango endelevu ya mfumo wa maji taka na hivyo kuzidiwa kwa chemba hiyo kunakotokana na ongezeko la idadi ya watu katika jiji la Dar es salaam.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine