Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watakiwa kupambana na mabadiliko ya tabia nchi

Jumanne , 7th Jun , 2022

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Khamis Hamza Khamis amewataka Wadau wa kilimo kuungana kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa kulinda na kuhifadhi misitu, vyanzo vya maji na rasilimali zote tegemeo la kiuchumi na kijamii.

Naibu Waziri Hamza Khamis amesema hayo wakati akishiriki kwenye Ufunguzi wa Kongamano la Nane la Mwaka la Sera kwa Wadau wa Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Alisema Tanzania ina utajiri mkubwa wa misitu ndani Mashariki na Kusini mwa Afrika ambako takribani hekta milioni 48.1 ni eneo la misitu lakini pamoja na hayo takribani hekta 469,420 hupotea kila mwaka kwa sababu ya shughuli za kilimo, makazi, shughuli nyingine za kijamii.

Khamis aliwaomba wataalamu kuona nanma ya kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi hasa kuni na mkaa kwa kuhamasisha matumizi ya majiko ya kupikia yanayotumia nishati vizuri na mkaa wa kisasa. 

“Niwaombe wadau wetu wa kilimo, mifugo na uvuvi muangalie teknolojia, mbegu, afya ya udongo, mbolea  na viuatilifu ambavyo kwenye sekta hii vinaweza kusaidia sana katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi,” alisema Khamis. 

Alisema sehemu nyingi hapa nchini ambazo zilikuwa zina misitu na uoto wa asili, zilikuwa zinapata mvua mara mbili hadi tatu kwa mwaka na sasa hivi zinapata mara moja na pengine hakuna kabisa na hivyo shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi katika maeneo hayo zimeathirika.

Hivyo, alisema upotevu huu wa miti husababisha pia ongezeko la hewa ya ukaa ambayo huchangia kuongezeka kwa joto ambapo inakadiriwa kuwa hadi mwaka 2080, joto hapa nchini litakuwa limeongezeka kati ya nyuzi joto 1.40C hadi 3.60C na kupungua kwa mvua hivyo kuathiri shughuli za kiuchumi zikiwemo kilimo, ufugaji na uvuvi.  

Naibu Waziri Khamis alisema Ofisi ya Makamu wa Rais imejipanga kuhakikisha Sera, Sheria, miongozo na Mikakati mbalimbali ya Kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi zinafanyiwa kazi.

Kongamano hilo la siku tatu  linalowashiriki wadau mbalimbali kutoka sekta za kilimo, mifugo, uvuvi na mazingira lina Kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika sekta ya mazao, mifugo, uvuvi na mazingira.

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria