Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TPA yapokea magari 4397 kwa pamoja

Jumanne , 10th Mei , 2022

Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imevunja rekodi kwa kupokea meli yenye magari 4397 ambayo yametoka nchini Japan na hivyo kuwa meli ambayo imepokelewa bandari ya Dar es salaam ikiwa na magari mengi zaidi. Awali, bandari ya Dar es salaam ilipokea meli yenye magari 4041 mwezi April 2022.

Sehemu ya magari 4397 yakiwa tayari yameshushwa bandarini

Mamlaka ya Bandari nchini Tanzania (TPA) imesema kuwa meli ya Meridian Ace ambayo imetia nanga katika bandari ya Dar es Salaam ikiwa na jumla ya magari 4397 kwasasa ndiyo meli ya kwanza kushusha magari mengi kwa pamoja katika historia ya bandari hiyo na TPA.

"Hii meli ya meridian ace imevunja rekodi kwa kuingiza magari 4397 kwa wakati mmoja, imevunja rekodi ya meli tuliyoipokea mwezi Aprili mwaka huu ambayo ilikuwa na magari 4041. Imetoka moja kwa moja nchini Japan lakini ilipita Singapore kabla ya kufika Tanzania"- Nicodemus Mushi, Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano - TPA.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa mamlaka ya bandari (TPA) Bw. Nicodemus Mushi amefafanua kwamba asilimia 23 ya magari hayo yanabakia nchini Tanzania huku asilimia 77 yakiwa ni ya mataifa nchi jirani. Ameongeza kuwa kupokea magari mengi kiasi hiki ni matokeo ya kuaminika kwa huduma za bandari ya Dar es salaam na kuwashukuru wadau kwa kuitumia bandari hiyo.

"Katika magari haya, 23% yanabakia nchini hapa na 77% ya magari haya yanakwenda nchi jirani ya Zambia, Malawi, Rwanda, Burundi, na Congo DR. Hii inamanisha kwamba wadau wetu wameendelea kuamini huduma za bandari ya Dar es salaam, lakini pia usalama, uharaka wa huduma na uaminifu" - Nicodemus Mushi, Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano - TPA

 

HABARI ZAIDI

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera