Jumanne , 5th Dec , 2023

Timu inayoshiriki ligi kuu nchini Uingereza EPL, Sheffield United imemfuta kazi Kocha wake Mkuu Paul Heckingbottom baada ya kutokuwa na matokeo mazuri msimu huu.

Sheffield imecheza jumla ya michezo 14 ya EPL na kupoteza michezo 11, kutoa droo michezo miwili na kushinda mmoja tuu dhidi ya Wolves mwezi Novemba.