Aishi Manula
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Simba SC, kupitia ukurasa wao wa Instagram umewkeka wazi kuwa goli kipa Aishi Manula yupo salama na ataruhusiwa kutoka hospital kwenda nyumbani hii leo baada ya kupata matibabu kwenye Hospitali ya Kairuki mikocheni.
Aishi Manula aliumia jana kwenye mchezo wa ligi kuu katika dimba la Benjamin Mkapa, wakati timu yake ikimenyana na JKT Tanzania, Kipa huyo aligongana na mchezaji wa JKT na kupoteza fahamu akiwa uwanjani kwenye mchezo amabao Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-0.
Lakini pia taarifa hiyo iliyotolewa na mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Simba SC Haji Manara iliweka wazi kuwa mchezaji huyo atakuwa sehemu ya kikosi kitakachoondoka nchini kesho kueleka nchini Sudan, ambako timu hiyo itacheza mchezo wa klabu bingwa Afrika dhidi ya Al Merrikh siku ya Jumamosi Machi 6, 2021.