Mlinda Mlango wa Azam FC, Aishi Salum Manula
Manula amesema bado ana mkataba na Azam FC utakaomalizika Julai mwaka huu, na hivi sasa yupo kwenye mazungumzo na viongozi wa Azam FC juu ya kuuongeza.
Kipa huyo namba moja wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, ameweka wazi kuwa mazungumzo hayo yanaendelea vizuri na anaamini atasaini katika timu hiyo iliyomtunza na kumlea vema hadi leo hii kuanzia kwenye academy yake hadi timu kubwa.