Jumatatu , 5th Feb , 2024

Klabu ya Yanga SC, inatarajia kuzindua ofisi zake katika makao makuu ya timu hiyo Februari 07, 2024 baada ya kufanyiwa ukarabati na maboresho,

Akizungumza na waandishi wa habari  Afisa habari wa klabu hiyo Ali Kamwe amesema ‘ofisi hizo  ni ofisi bora za timu ya mpira wa miguu Afrika Mashariki na kati.

"Ratiba ya tarehe 11 Fabruari tutakuwa Mbeya kwenya mechi dhidi ya Prisons, ambapo birthday yetu itakwenda kufanyika Mbeya. Mkoa wa Mbeya umepata Bahati ya kusheherekea historical Anniversary ya Klabu kubwa katika historia ya mpira wa Tanzania"

"Tunakwenda kuzindua nyimbo mbili kubwa kwa lengo la kusheherekea kilele cha anniversary ya mabingwa wa kihistoria. Yaani kuelekea kwenye hiki kilele ni jiwe juu ya jiwe. Hakupoi, kila mwanachama anapaswa kuweka kambi Mbeya."amesema kamwe.