Jumatatu , 29th Jan , 2024

Kocha Mkuu wa Simba SC, Abdelhak Benchikha amesema usajili ambao wameufanya unakwenda kurudisha makombe ambayo waliyapoteza katika katika kipindi cha msimu miwili

"Tumeanza mazoezi kwa ajili ya kujiweka sawa kwenye ligi kuu pamoja na CAF Champions League, Tumefanya usajili nimeona Simba SC ya kesho ni nzuri kwa mashabiki na kwa wapenzi wote wa klabu."- amesema Benchikha.

Kikosi cha Simba SC kimeshaingia kambini tayari kwa maandalizi ya michezo ya ligi kuu Tanzania Bara na Klabu bingwa barani Afrika.