Wachezaji hao baada ya kusaini mikataba mipya
Arsenal haijatoa muda wa mikataba ya wachezaji hao wa Kifaransa, lakini beki Koscielny aliandika kwenye mtandao wa Twita kuwa ataitumia the Gunners hadi 2020.
Wafaransa hao wote watatu wamekuwa nguzo muhimu kwa Arsenal kwa sasa, ambapo Giroud amekuwa gumzo kwa kufunga mabao manne katika michezo minne iliyopita, kujumuisha na bao la kiufundi 'Scorpion Goal' alilofunga hivi karibuni kwenye mchezo dhidi ya Crystal Palace.