Jumatano , 24th Jan , 2024

Chama cha Soka nchini Ghana (GFA) imemfuta kazi mkufunzi wake mkuu Chris Hughton baada ya Ghana kuondoshwa kwenye hatua ya makundi ya michuano ya Afcon 2023 nchini Ivory Coast.

Taarifa ya GFA imesema Chris Hughton ameondoshwa kwenye majukumu yake kama kocha mkuu wa Ghana na kamati ya utendaji imechukua uamuzi wa kuvunja benchi lote la ufundi la Black Stars

Mkufunzi Chris Hughton aliteuliwa kuwa mshauri wa ufundi ndani Ghana 2022 kabla ya kutangazwa kuwa kocha mkuu wa Ghana mnamo Februari 2023 akichukua nafasi ya Otto Addo aliyejiuzulu baada ya fainali za kombe la Dunia 2022