Jumatano , 27th Oct , 2021

Familia ya Gwenny Blanckaert na   Marino Vaneeno imekuwa na utamaduni wa kipekee linapokuja suala la kuwapa majina watoto wao

Picha ya familia ya Marino Vaneenoo na Gwenny Blanckaert

ambapo  familia hiyo yenye jumla ya watoto 11 ( wa kike 7 na wa kiume  4) imekuwa ikitumia herufi 4 zinazofanana katika kuwapa majina watoto wao wote 11, na  herufi hizo ni (A , X ,E na L).

Mtoto wa kwanza katika familia hiyo ni  Alex ana miaka 13, akifuatiwa na Axel,( 12), Xela, (11), Lexa,( 10), Xael, (9), Xeal, (8),Exla, (5), Leax,( 4),  Xale, (2), Elax,(1), na Alxe ambaye ana miezi 6.

Hivi karibuni wazazi hao wanatarajia kupata mtoto wao wa mwisho wa kiume mwezi Aprili mwaka 2022 ambaye atakamilisha idadi ya wototo 12.