Vidonge hivyo vitafanyiwa majaribio kwa wanaume mwishoni mwa mwaka huu.
Tangu kidonge cha kuzuia mimba kwa wanawake kilipogunduliwa, wanasayansi waliendelea kufanya utafiti kwa upande wa wanaume ili watu wote wawe na jukumu sawa la uzazi wa mpango.
Kidonge hicho kitapunguza uwezo wa mwanaume kumpa mimba mwanamke kwa muda, na kitafanyiwa majaribio kwa wanaume mwishoni mwa mwaka huu.