Jumanne , 30th Nov , 2021

Mwanamziki Rihanna ameandika historia mpya siku ya leo baada ya kutangazwa kuwa shujaa wa taifa la Barbados katika tukio kubwa la taifa hilo kutangazwa kuwa serikali huru inayojitegemea baada ya kuwa chini ya utawala wa Malkia Elizabeth wa Uingereza kwa zaidi ya miaka 55.

Picha ya msanii Rihanna

Rihanna alichaguliwa kuwa balozi wa visiwa vya Barbados mwaka 2018, leo ameingia katika list ya mashujaa wa taifa hilo jipya Duniani likijitegemea kama Jamhuri kwa mara ya kwanza. 

Dame Sandra Mason amechaguliwa kuwa rais wa kwanza wa Barbados amemtangaza Rihanna kuwa shujaa wa taifa hilo kwa mchango wake mkubwa katika kulitangaza taifa hilo kupitia kazi zake za sanaa na amefanya watu wengi kuvijua visiwa vya Barbados.