Jumamosi , 31st Jan , 2015

Mastaa wa muziki kutoka nchini Uganda, Radio pamoja na Weasel wameelezwa kuwa katika mpango wa kusaka meneja mpya ambaye ataenda nao sawa na kuhakikisha anawaweka sawa katika kuimarisha soko la muziki wao nje ya mipaka ya nchi hiyo.

Weasel na Radio

Hatua hii imeelezwa kuwa ni kutokana na kitendo cha meneja wao wa sasa anayefahamika kwa jina Chagga kuteleza na kuingia katika ugomvi na mashabiki wa wasanii hawa, kitendo ambacho wanahofia kuwachafulia jina na kuyumbisha biashara yao ya muziki.

Wasanii hawa pia wameweka mkakati huu kwa lengo la kwenda sawa na kasi ya ushindani ya muziki ambao sasa umekuwa na unahitaji kusambaa kwa kasi nje ya mipaka ya nchi yao.