Jumamosi , 12th Sep , 2020

Msanii wa BongoFleva Nay wa Mitego ameeleza kuwa yupo tayari kutoa wimbo mpya kwa sasa kutokana na watu wengi kumuuliza maswali kuhusiana na ujio wake ambapo mara ya mwisho alitoa kazi ya yupo wapi.

Msanii wa BongoFleva Nay Wa Mitego

Nay wa Mitego amefahamisha hilo kupiti ujumbe aliouweka kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram ambao umefuatana na comments mbalimbali kutoka kwa wadau na mashabiki wa muziki huku wakihitaji atoe wimbo mpya.

Kupitia post hiyo Nay wa Mitego ameandika kuwa  "Sawa nipo Tayari kuwapa ngoma mpya mmenidai sana, HashTag ni Haki, Haki, Haki. Comments 600 naachia ngoma".