Koffi Olomide na Nandy
Nandy pia ameonesha kutambua kiu ya mashabiki wake kwenye kuisubiri video hiyo ya #Leoleo na kupitia page yake ya Instagram amekutana na Koffi ambapo amepost video akidokeza kuwa maongezi yake na Koffi ilikuwa ni juu ya kuachia video hiyo. Hata hivyo bado hajaweka wazi ni lini ataiachia.
''Hapa anasema mbona siachii VIDEO? Nikamwambia tulia MOPAO watu hawana haraka wanaruka rumba'', ujumbe alioandika Nandy kwenye video fupi aliyopost akiwa na Koffi.
Audio ya Collabo hiyo imepandishwa YouTube siku ya Feb 11, 2021 na mpaka sasa imetazamwa zaidi ya mara laki tano.