Picha ya Mkalimani Matungwa Mutatina
Akipiga stori na EATV & EA Radio Digital, Mkalimani huyo amesema mitambo ilifika mahala ambapo sauti inatoka ikiwa inakatakata kisha akawa hasikii kabisa sauti inayotoka kwa aliyekuwa anaongea.
"Ile hali ilinistua kidogo, kilichokuwa kimetokea haikuwa kwamba nimeshindwa kutafsiri maneno ila kulikuwa na sababu za kiufundi, mitambo ilifika mahala ikawa haisikii na sauti inakuja kwa kukatakata lakini haikunivunja moyo, kwa sababu waliokuwa wanacheka hawakujua kilichotokea na kuendelea" ameeleza Mkalimani Matungwa Mutatina
Aidha Mkalimani amesema anawaomba watu wawe na uzalendo na wajirekibishe kwa kilichotokea kwa sababu kulikuwa na vitu vingi hasa ilikuwa siku ya kumuaga Hayati Dkt John Pombe Magufuli ila watu wamemdhihaki na kumcheka kwa kilichomtokea.
Zaidi mtazame hapa chini.