Alhamisi , 23rd Nov , 2017

Star wa Bongo Fleva Cyril Kamikaze amefunguka kupitia eNEWZ kuhusu tuhuma zinazomkabili za kumzalilisha mpenzi wake Feza Kessy kwa kuanika picha inayoonyesha matiti yake katika mtandao wake wa instagram.

Kamikaze amesema haoni tatizo lolote la ile picha kwani ni picha  ya kawaida sana na haijaonyesha kiungo chochote cha Feza anachojua ni kwamba picha ile inaonyesha sehemu kidogo ya matiti  ya Feza ambapo ni sawa tu na wanawake wanaovaa brazia kuyabusti maziwa yao ili yaonekane.

Hata hivyo Kamikaze amesema hawezi kumdhalilisha Feza kwani anamuheshimu sana na Feza ndo alipiga ile picha na kumtumia yeye na hata alipoipenda na kuamua kuipost katika mtandao wake wa instagram alimpigia Feza kumuambia kuwa anaipost na Feza alikubali bila wasiwasi

Kamikaze amemalizia kwa kusema kuna wasanii wengi wanapiga picha za utupu zaidi hata ya ile mbona watu hawashangai?anamalizia kwa kusema watu wanapaswa kufahama kwamba Feza ni msanii na anapaswa kupiga picha za aina ile ilimradi hayupo uchi.