Jumatano , 17th Apr , 2024

Msanii Tiwa Savage afichua kwamba alianza kupenda kuigiza kabla ya kufanya muziki lakini ‘Crush’ wake muda wote ni mtu wa muziki akambadilsha mawazo.

Picha ya Tiwa Savage

Tiwa Savage ameshea hilo akizungumzia ujio wa Movie yake mpya ya Water & Garri itakayotoka siku ya May 10, 2024.

“Muda wote nilikuwa nataka kuigiza, ndio nilikuwa napapenda kwanza kabla ya muziki. Niliingia kwenye muziki sababu Crush wangu alikuwa karibu na wanamuziki nikasahau tena kuigiza nikaingia kwenye muziki” amesema Tiwa Savage

Pia amempa mashavu msanii mwenziye wa kike nchini Nigeria Simi kama ndio Malkia wa muziki wa Afrobeats.