Jumamosi , 5th Dec , 2020

Mchekeshaji anayefanya vizuri kwa sasa kwenye mitandao ya kijamii Chikumbalaga Sukariyao ametoa kali ya mwaka baada ya kuanza kutembea na 'bodyguard' wake mtaani kama wanavyofanya baadhi ya wasanii.

Mchekeshaji Chikumbalaga Sukariyao akiwa na bodyguard wake

Mchekashaji Chikumbalaga Sukariyao ambaye anatokea Tunduma Mkoani Mbeya, ameweza kutrend mitandaoni baada ya kushea picha hizo akiwa na bodyguard wake kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Aidha Sukariyao huyo amepata umaarufu kwa njia ya wasanii kumtumia kwenye upande wa kuchekesha pale anaposhea video na audio akizisapoti kwa kucheza au kuimba nyimbo za wasanii hao kisha kupost mitandaoni.

Zaidi tazama hapa kwenye picha akiwa na bodyguard wake.