Jumamosi , 21st Oct , 2017

Mrembo aliyejipatia umaarufu hivi karibuni kwa kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na msanii Dulla Makabila anayejulikana kwa jina la Asali, amekiri kutoa ujauzito ambao alipewa na msanii huyo.

Akiongea kwenye Friday Night Live ya East Africa Television, Asali amesema ni kweli mimba hiyo ametoa kwa sababu aliona Dulla hana msimamo juu yake tangu alipopata ujauzito.

"Kweli nilikuwa nao ujauzito na nikautoa mimi mwenyewe, niliona bado anayumbishwa na maamuzi yake, alikasirika na alitaka kunipiga tena baada ya kujua kuwa mwanamke wake hana mimba", alisikika Asali akimwambia Sam Missago wa FNL.

Tazama interview yote hapa chini