Msanii Barnaba Classic
Dongo hilo Barnaba ameliweka kwenye ukurasa wake wa Instagram baada ya mzazi mwenzke huyo kudai kuwa baada ya miaka mtano kupita hatimaye sasa amefanikiwa kupata amani ya moyo ambayo ndicho kitu alichokuwa akikikosa kwa muda wote.
Barnaba ameandika "Mama aliniambia ukimtukana mwanamke basi umenitukana na mimi. Siku zote nawaona kama mama zangu hongera wanawake wote duniani Salamu zangu juu yenu Jumapili ya leo nawapenda Sana"
Ujumbe wa Barnaba aliouweka Instagram leo hii baada ya ujumbe wa Mzazi mwenzake
Mzazi mwenzake Barnaba, Zuu Namela ambaye walibahatika kupata mtoto wa kiume 'Steve' leo asubuhi aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kisha kufuta ujumbe huu.
"Ni watu wachache sana wanaojua nikitu gani nilikua nakosa katika maisha yangu! Unaweza ukapata kila kitu kwenye maisha ila ukakosa furaha,amani,heshima......kwa zaidi ya miaka mitano hichi ndo nilicho kuwa nakitafuta #AMANIYAMOYO "
Ujumbe wa mzazi mwenzake Barnaba, Bi Zuu Namela kabla ya kuufuta.