Msanii wa BongoFleva Alikiba
Alikiba amesema hayo kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio mara baada ya kuulizwa kwanini ametoa wimbo wa aina hiyo wakati hawamjazoea akifanya miziki ya aina hiyo.
"Muziki una season na mimi nnimeona huu ndiyo wakati wake nilisemaga nikianza kujibu mtashangaa maana tukipiga kelele tutakuwa wote wajinga halafu hatutasikilizana ila baadaye nikitulia nitakupa jibu lako na sipo kwa ajili ya ushindani"
"Baada ya kuachia hii ngoma nilienda mahali kula mitaa ya Upanga ambapo watu wanaouza hapo nawafahamu, sasa kuna kijana mmoja ni cashier pale, baada ya kula wakati naondoka akawa ananiongelea vibaya sana hadi nikapigiwa simu kupewa tahadhari nisiende kula tena pale, maana naweza kuekewa hadi sumu kwa jinsi ambavyo alikuwa ananiongelea, najua watu hawanipendi lakini mimi sijali" ameongeza