Kanisa lililoanguka mkoani Katavi
Taarifa hiyo imetolewa leo Novemba 20, 2020, na Kamanda wa polisi mkoani humo, Benjamini Kuzaga, ambapo amesema kuwa chanzo cha maafa hayo ni mvua kubwa iliyonyesha ikiwa imeambatana na upepo mkali, hali iliyopelekea kulowa kwa kuta za kanisa hilo na kisha kuanguka.
Akiendelea kutolea ufafanuzi wa maafa hayo Kamanda Kuzaga amesema kuwa kati ya watu 18 waliojeruhiwa 7 ni watoto na 11 ni watu wazima.
Jeshi la Polisi mkoa wa Katavi, limewaasa wananchi kuwa makini katika kipindi hiki cha msimu wa mvua kwa kuchukua tahadhari katika makazi wanayoishi.