Ijumaa , 30th Oct , 2020

Msanii wa HipHop Webiro Wasira 'Wakazi' ameshindwa kuchukua nafasi ya Ubunge ambalo alikuwa anagombea Jimbo la Ukonga kupitia Chama Cha ACT-Wazalendo ambalo limeenda kwa mshindi Jerry William Slaa kutoka Chama Cha Mapinduzi.

Msanii na aliyekuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Ukonga Wakazi Webiro Wasira

Kwa mujibu wa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Ukonga amemtangaza Jerry William Slaa wa CCM kukalia kiti cha Ubunge baada ya kupata kura 120936 sawa na asilimia 81.2 na msanii Wakazi Webiro Wasira kutoka ACT-Wazalendo amepata kura 2087 sawa na asilimia 1.4

Aidha Jimbo hilo la Ukonga kutoka Halmashauri ya Manisapaa ya Ilala lilikuwa na jumla ya wagombea Ubunge 18.