Ijumaa , 21st Oct , 2016

Uzalishaji wa mvinyo unatarajiwa kuendelea kushuka kwa miaka minne mwaka huu, kufuatia hali mbaya ya hewa kuathiri uzalishaji wake katika mataifa ya Ufaransa na Amerika ya Kusini.

Zabibu moja kiati ya mazao yayotumika kutengenezea mvinyo

 

Shirikisho la Kimataifa la Biashara ya Mvinyo (OIV), linakadiria uzalishaji wa mvinyo kufikia hektolita milioni 259.5 mwaka huu, ikiwa ni kushuka kwa asilimia 5 ikilinganishwa na mwaka jana.

Shirika hilo limesema mwaka huu utakuwa wenye uzalishaji duni wa mvinyo kuwahi kutokea tangu mwaka 2000, lakini limesema hali hiyo haitoathiri bei ya mvinyo duniani.