Takwimu hizo ni kwa mujibu wa taarifa ya mwenendo wa biashara katika soko hilo kwa kipindi cha wiki moja iliyopita kipindi ambacho mtaji wa kampuni za ndani nao ukiwa umepungua kwa Shilingi Bilioni 150 kutoka Shilingi Trilioni 7.21 wiki iliyopita hadi Shilingi Trilioni 7.06 wiki hii.
Aidha katika kipindi hicho, mauzo ya hati fungani yameongezeka kutoka mauzo yenye thamani ya Shilingi bilioni 22.6 hadi Shilingi bilioni 29.5; hii ikiwa ni kutokana na mauzo ya hati fungani tisa za serikali na hati fungani moja ya EXIM zenye jumla ya thamani ya Shilingi bilioni 39.5 kwa jumla ya gharama ya Shilingi bilioni 29.5.