Pichani raia wa kigeni waliokamatwa
Akielezea kukamatwa kwa raia hao wa kigeni jana kaimu afisa uhamiaji mkoa wa Kigoma Kamishna msaidizi wa uhamiaji Augustino Matheo amesema raia hao wamekamatwa baada ya msako uliofanyika February 05 na 06 katika maeneo mbalimbali mkoani Kigoma uliofanikisha kukamata raia 43 kutoka nchi ya Burundi kati ya wakiwemo wakimbizi 3 na raia 9 kutoka nchi ya kidemokrasia ya Kongo ambao ni wakimbizi kutoka kambi ya Nyarugusu.
Pia Matheo ameeleza kuna watanzania watatu waliokuwa wakiwatumikisha raia hao nao wamekamatwa na baadae watafikisha mahakamani pamoja na wahamiaji hao .