Jumatano , 30th Mar , 2016

Rais Magufuli amesema kuwa amepanga kupangua upya mishahara mikubwa ya wafanyakazi wanaopokea hadi shilingi milioni 40 na kusema kuwa lengo lake ni kuhakikisha katika kipindi chake kusikuwepo watu wanaolipwa zaidi ya shilingi milioni 15 kwa mwezi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli

Akiongea na Wananchi katika Mkutano wa hadhara wilayani Chato, Mkoani Geita, Rais Magufuli ametolea mfano wa mfanyakazi mmoja wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) ambaye alikuwa akilipwa mishahara ya watu 17, na kueleza kuwa mfanyakazi huyo atafikishwa mahakamani.

Pia Rais Magufuli amesema serikali yake imejiandaa kuboresha maslai ya wafanyakazi kwa kupunguza kodi kutoka asilimia 11 ya sasa hadi asilimia 10 au 9 kuanzia bajeti ijayo,

Rais Magufuli amesema kwa wale wanaolipwa mishahara mikubwa ambayo inafikia hadi shilingi milioni 40, itapunguzwa na kuweka kima cha juu cha mshahara usiozidi shilingi milioni 15.

Kuhusu tatizo la wafanyakazi hewa, Rais Magufuli amesema uhakiki mdogo uliofanywa hivi karibuni, umebaini wafanyakazi hewa 1,680 waliokuwa wakilipwa shilingi bilioni 1 na milioni 800, na kwamba ni matarajio kuwa uhakiki unaofanywa nchi nzima utaisaidia serikali kubaini wafanyakazi hewa wengi zaidi na kunusuru fedha nyingi zaidi za watanzania.

Sauti ya rais Magufuli akizungumzia mtu anaelipwa kwenye akaunti 17
Sauti ya Magufuli malengo ya kupunguza mishahara ya wanaolipwa milioni 40