Kiwanda cha mataruma cha Kongolo Mbeya
Kiwanda hicho ambacho ni mali ya TAZARA, kilianzishwa tangu mwaka 1977, kwa ubia na nchi ya Uchina na tangu kipindi hicho mitambo yake haijabadilishwa wala kufanyiwa ukarabati, licha ya kuwa na umuhimu mkubwa.
Juma Mizambwa ni Kaimu Meneja wa Kiwanda hicho anafafanua (Sikiliza sauti yake hapa chini)
Kamati ya Bunge inayoshughulikia miundombinu nchini ikiongozwa na Mwenyekiti wake Prof. Norman Sigalla, imetembelea kiwanda hicho, na kutoa mapendekezo yake kukinusuru kiwanda hicho (Sikiliza sauti za wabunge hapo chini)
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Meneja Mkuu wa Tazara kwa upande wa Tanzania, Fuad Abdallah imedai kuwa shilingi bilioni 3.5 zinahitajika kununulia mitambo mipya au bilioni 2.2 kufanya ukarabati. (Sikiliza sauti hapa chini)
Nao baadhi ya wadau waliotembelea kiwanda hicho ambao ni wabunge akiwemo Zubery Mchauka na Anna Lupembe wametoa maoni yao (Sikiliza sauti hapa chini)