Rais Magufuli akiwa na Mwenyekiti Mtendaji wa Bodi ya migodi ya dhahabu ya Barrick, John L. Thornton
Taarifa hiyo ambayo ni mara ya kwanza kutokea kwenye historia ya Tanzania, imetolewa leo na serikali wakati ikikabidhi ripoti ya mazungumzo hayo kwa Rais John Pombe Magufuli, na kusema kwamba licha ya makubaliano hayo, pia kampuni hiyo imekubali masharti yote yaliyowekwa kufuatia mazungumzo hayo, ili nchi iweze kunufaika na rasilimali zake.
Pia kwenye ripoti hiyo imekubaliwa kuwa migodi yote itaweka fedha zake kwenye akaunti zilizopo hapa nchini, na serikali kubakia na umiliki wa madini yote yatakayokuwepo kwenye makinikia, ukiondoa dhahabu, shaba na fedha ambayo yatakuwa yanamilikiwa na Barrick kisheria.
Pamoja na hayo makubaliano yaliyofikiwa yameitaka kampuni hiyo kuwapa ajira za kudumu wazawa wa eneo husika, na kuwapa stahiki zote kama wafanyakazi, na wamekubali kulipa kile kinachostahili kwenye halmashauri husika ambako migodi ipo.
Kufuatia ripoti hiyo Rais Magufuli ameipongeza timu iliyohusika kwenye mazungumzo hayo, na kuwataka Watanzania kushirikiana katika kuleta maendeleo ya nchi.