Bodaboda
Wakizungumza viongozi wa bodaboda wilayani hapo wamesema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 2:00 usiku na kusema wizi na vifo vya madereva bodaboda havitakwisha kama jeshi la polisi halitadhibiti wanaojiita deiwaka wanaojitokeza nyakati za usiku kwani ndiyo chanzo cha wizi kwa kuwa hawajasajiliwa kwenye uongozi wao na hivyo hata wakifanya tukio hawawezi kuwatambua.
Aidha wakazi wa mtaa huo wamesema kwa sasa vitendo vya mauaji katika mtaa wao vimekithiri jambo ambalo sio la kawaida.